Viongozi wa dini za Kikristo na Kiislam wametakiwa kutumia vema
nyadhifa na fursa walizonazo katika kuhakikisha kuwa waamini wao
wanadumisha Amani na Utulivu Nchini ikiwa ni pamoja na kuwaunganisha
waumini wao bila kujali mipasuko mbalimbali inayojitokeza hapa nchini.
Wito huo Umetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa, Mhe Bernard Membe baada ya Misa iliyoambatana na uwekaji wa
jiwe la msingi la ujenzi wa hosteli ya kanisa katoliki parokia ya
Nachingwea sambamba na uzinduzi wa Kitabu cha maandiko ya sehemu ya
bibilia iliyotafsiliwa kwa lugha ya kabila la Kimwera.
Mhe
Membe alibainisha kuwa hali inayojitokeza hivi sasa inaweza kukomeshwa
iwapo viongozi wa dini watakuwa msitari wa mbele kuwaelimisha waumini
wao madhara ya ukosefu wa amani na Kutokubali kurubuniwa na kuwa
vyanzo vya uvunjifu wa amani.
Awali akisoma taarifa ya Umoja wa Makanisa ya kikristo
Nachingwea,Mchungaji wa EAGT,Pius Mnombela alieleza kuwa Umoja huo
umefanikiwa kutafsiri vitabu vyote vya agano jipya ambapo vitabu vya
Injili ya Luka na Marko vimefanyiwa ukaguzi wa awali na kubainisha
lengo la kuanzisha Mpango wa Kuanzisha Utafsri huo na uzinduzi wa
kitabu cha Biblia kwa Lugha Asili ya Kimwera .
Naye Fr Ngombo wa kanisa hilo aliwataka waumini kuchangia
Parokia zao kufuatia Makanisa Mengi kukosa wafadhili wa Nje ambapo
katika Harambee Iliyoendeshwa na Waziri Membe na kufanikisha
kuchangiwa kiasi cha shilingi milioni 31 kati ya fedha hizo Waziri
huyo alichangia shilingi milioni 10 pia aliahidi kuhakikisha Jengo
hilo linakamilika kama lilivyokusudiwa kufuatia Nguvu kubwa
zilizoonyeshwa na waumini mbalimbali
Uzinduzi huo wa Biblia ya Kimwera,Uwekaji wa Jiwe la Msingi na
Harambee ya kukamilisha ujenzi wa Hostel ya Parokia hiyo umefanikiwa
kushirikisha makundi mbalimbali bila kujali Itikadi zao za imani na
udhehebu na kuwezesha kupata Tafsiri sahihi ya Biblia kwa Lugha ya
Kimwera lugha ambayo utumika na wakazi wengi wa Wilaya za
Ruangwa,Lindi na Nachingwea Mkoani LINDI
Moja ya kurasa za kitabu cha maandiko ya sehemu ya bibilia iliyotafsiliwa kwa lugha ya kabila la Kimwera.
Mhe Bernard Membe akizindua Kitabu cha maandiko ya sehemu ya bibilia iliyotafsiliwa kwa lugha ya kabila la Kimwera.
Vifijo baada ya uzinduzi wa kitabu hicho
Fr. Ng'ombo akiongea wakati wa hafla hiyo
Mhe Membe akifunua pazia kama ishara ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hosteli ya kanisa katoliki parokia ya Nachingwea
Kanisa Katoliki parokia ya Nachingwea kwa nje
Mhe Bernard Member akihutubia waumini
Mhe Bernard Membe akiwa kanisani humo
Waumini wakiwa katika misa hiyo
Kasusula ni msaidizi wa Membe siku hizi?
ReplyDeleteHiyo ndio itakua lugha ya taifa kusini?
ReplyDeleteMmmh kazi ipo!Ila baba alikua hapendi mchezo huu....bahati yenu hayupo.
ReplyDelete