Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Mwananchi,Mwanja Ibadi pamoja na
Diwani wa kata ya Kikole,Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa,Mkoani Lindi,Haji Mulike wamenusurika kupoteza maisha katika ajali waliyoipata,wakiwa njiani kuelekea Wilayani Nachingwea,kwa shughuli za kikazi.Katika ajali
hiyo mtu mmoja alipata majeraha Madogo.Picha na Abdullaziz Video
Gari walilokuwa wakisafiria Wadau hao likiwa limepinduka huku huzuni ikitawala katika eneo hilo.
barabara mbovu hiyo; na inaonekana inatokea lindi (mkoani) kwenda nachingwea (wilayani). Yani barabara kama inaenda shambani (mashamba ya kwetu TZ) manake kwa wenzetu barabara za kwenda shambani ni kama barabara ya kutoka lindi kwenda dar. Kwa barabara hizi maisha yetu yatakuwa hatarini tu. Poleni Watanzania wenzangu, yatakwisha...
ReplyDeletembunge wa jimbo hili ninani?na linaongozwa na serikali gani ?barabara mbaya namna hii?okay nawapa pole wahanga wa ajali na nawasihi wakatoe sadaka ya shukrani kwa Mungu .
ReplyDeletePoleni sana Ndugu Diwani na mwandishi na familia zenu..Pamoja na barabara kua mbovu inaonekana hawa walikua pia speed sana.
ReplyDeletehio barabara ukiwa mwendo wa kawaida cdhnani kama utaweza kupinduka na gari matairi yakawa juu.
kinanisikitisha ni hao watoto hapo. Hata kama barabara ni mbovu vipi, ni swala la dereva kuamua anaendesha ili wafike salama au ndio ule ule ujinga wa kutosomea kuongoza vyombo vya moto ndio unatawala. Hiyo barabara ninavyoangalia sio ya kupindua hilo gani ujinga tu ndio utakuwa umetawala kwa huyo dereva. Nimeendesha gari tanzania miaka mingi sana.
ReplyDeletePoleni watoto.