Bondia kijana na anayeinukia kwa kasi Albinu Felesianu wa nchi ya Namibia amepewa ofa ya kugombea ubingwa wa dunia wa Featherweight kwa vijana walio chini ya miaka 25 unaotambuliwa na IBF. Albinus amezoea kupewa zawadi za Christmas na siku kuu yake ya kuzaliwa lakini hamna kilichomwandaa na mshtuko mkubwa ambao aliupata wakati IBF ilipotangaza hivi karibuni kuwa imempatia nafasi ya kugombea mkanda wa dunia kwa vijana walio chini ya miaka 25.

Mtua ambaye anaweza kuiua furaha yake ni mmoja wa watoto wa Nkrumah, Mghana Ishmael Ayeetey ambaye amekulia katika moja ya viunga vinavyosifika kwa kutoa mabingwa wa ngumi wa dunia kama kina Azumah Nelson, Joseph Agbeko na Ike Quartey.

Albinus Felesianu kulia akimrushia ngumi mpinzani wake kushoto


Mpambano huo utafanyika katika jiji la Windhoek nchini Namibia tarehe 29 March chini ya kampuni ya Kinda Boxing promotions ya bwana Kinda Nangolo!

Hili litakuwa pambano la pili la ubingwa wa dunia kwa vijana baada ya bondia Ilunga Makabu wa Jamhuri ya Watu wa Kongo (DRC) kumtwanga bondia Gogito Gorgiladze wa Georgia jijini Johannesburg nchini Afrika ya Kusini jumamosi iliyopita.

ISSUED BY:
INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA) 
DAR-ES-SALAAM, TANZANIA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...