Sign in to confirm you’re not a bot
This helps protect our community. Learn more
MTUHUMIWA WA UTEKAJI WA MTOTO APIGWA RISASI AKIJARIBU KUTOROKA
5Likes
919Views
Mar 102025
Dar es Salaam. Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam inamshikilia Stanley Bulaya, mkazi wa Kata ya Nguruka, wilayani Uvinza, Mkoa wa Kigoma kwa tuhuma za  kumteka mtoto wa kiume (8)  mwanafunzi wa Shule ya  Msingi Mbezi ya  jijini Dar es Salaam. Tukio hilo la utekaji lilifanyika Machi 6, 2025 eneo la Mbezi Luis, Wilaya ya Ubungo, mtoto huyo alipokuwa anaelekea shuleni baada ya kushushwa na baba yake mzazi kwenye kituo cha daladala jirani na anaposoma. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Jumapili Machi 9, 2025 Kamanda wa kanda hiyo, Jumanne Muliro amesema siku hiyo mtoto hakurudi nyumbani hadi saa moja jioni wazazi wake walipoanza kumtafuta huku wakiwasiliana na mwalimu aliyepigiwa simu na mtuhumiwa kutaka namba za wazazi.

Mwananchi Digital

1.16M subscribers