Na Benedict Liwenga-WHUSM.

Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye leo ametembelea Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam ili kukagua shughuli za marekebisho ya miundombinu inayoendelea uwanjani hapo ikiwemo kukagua ufanisi wa Kamera za kufuatilia matukio Uwanjani pamoja na marekebisho ya viti vya kwenye majukwaa.

Katika ziara yake Waziri Nape amekagua namna Kamera za CCTV zinavyokuwa na uwezo wa kubaini matukio mbalimbali yanayoendelea uwanjani ambapo ameridhika na utendaji kazi wa kamera hizo na kusisitiza zitumike ipasavyo ili kuwabaini wahusika wanaoharibu miundombinu ya uwanja.

Amesema kwamba kazi ya kubaini waharibifu wa miundombinu kwa sura katika uwanja huu kwa kutumia hizi kamera yataongeza hali ya usalama kwenye uwanja na pia kusaidia kufuatilia matukio ya kihalifu Uwanjani kama vile kuvunja viti”, alisema Mhe. Nape.

Aidha, amesema kwamba ukarabati wa uwanja unaoendelea sasa pinid utakapokamilika utaufanya uwanja huo kuwa salama zaidi na ndiyo maana kamera nyingi zimeweka ili kuendelea kubaini matukio yanayoendelea ndani na nje ya mipaka ya uwanja ikiwemo milangoni.

“Kwa sasa uwanja wetu utaweza kushughulika na mtu mmoja mmoja anayehujumu miundombinu yetu, kwasababu kamera zetu zina uwezo mkubwa wa kumtambua mtu kwa sura pindi awapo uwanjani kuanzia magetini”,alisema Mhe. Nape.

Ameagiza ukarabati wa miundombinu uendelee ikiwemo mageti na viti uendelee kufanyika kwani yeye anachosubiria ni kukabidhiwa uwanja huo siku ya tarehe 13 Desemba mwaka huu na siku hiyo ndiyo itafahamika thamani ya ukarabati uliofanyika kwa ujumla.
Kaimu Meneja wa Uwanja wa Taifa Bw. Julius Mgaya (kushoto) akimuonyesha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye jinsi Kamera za CCTV zinavyoweza kumnasa mtu akifanya jambo lolote baya ndani ya Uwanja wa Taifa wakati alipotembelea kukagua marekebisho ya miundombinu ya uwanja huo leo 11 Desemba, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye, Kaimu Meneja wa Uwanja wa Taifa Bw. Julius Mgaya pamoja na Waandishi wa habari wakiangalia hatua iliyofikiwa ya urekebishaji wa viti na miundombinu mingine ya uwanjani hapo wakati alipotembelea kukagua marekebisho ya miundombinu ya uwanja huo leo 11 Desemba, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye (kulia) akiwa ameongozana na Kaimu Meneja wa Uwanja wa Taifa Bw. Julius Mgaya pamoja na Waandishi wa habari wakielekea kuangalia hatua iliyofikiwa ya urekebishaji wa viti na miundombinu mingine ya uwanjani hapo wakati alipotembelea kukagua marekebisho ya miundombinu ya uwanja huo leo 11 Desemba, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye akiangalia namna Kamera za CCTV zinavyofanya kazi ya kubaini matukio yanayoendelea ndani ya Uwanja wa Taifa wakati alipotembelea kukagua marekebisho ya miundombinu ya uwanja huo leo 11 Desemba, 2016 Jijini Dar es Salaam.

SOMA HAPA ZAIDI

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...