Kulia ni Dkt Ferdinand Masau, enzi za uhai wake, akimuonesha mgeni toka Texas Childrens Hospital ya Marekani  baadhi ya vifaa katika taasis yake ya Dr Ferdinand Masau Heart Institute aliyokuwa ameianzisha na kuanza kujenga  huko Mbweni Mpiji nje kidogo ya jiji la Dar es salaam. Hii ilikuwa Oktoba mwaka jana

Mtaalamu wa magonjwa ya moyo  Dkt. Ferdinand Masau, amefariki dunia  usiku wa kuamkia jana akiwa katika Hospitali ya Aga Khan, iliyopo Upanga jijini Dar es Salaama alikokuwa anatibiwa.
Habari hizo zimethibitishwa na marafiki wa karibu wa daktari huyo bingwa ambao hata hivyo hawakuwa tayari kutajwa majina kwa maelezo kuwa, wasemaji wa tukio hilo ni wanafamilia.
Maelezo kama hayo yalitolewa pia na mmoja wa maofisa wa hospitali ya Aga Khan, akisema wanafamilia ndio wanaoweza kuzungumzia taarifa za kifo cha mpendwa wao.
Enzi za uhai wake, baada ya kufanya kazi kwa miaka kadhaa nje ya nchi, alirejea nchini mwanzoni mwa miaka ya 2000 na kuanzisha taasisi ya moyo, akilenga kuwasaidia Watanzania wengi ambao kwa muda mrefu walikuwa wakikosa tiba ya uhakika nchini, hivyo kukimbilia nje ya nchi, hasa India.
Hata hivyo, ndoto zake ziliyumba kwa kiasi fulani kutokana na kukosa majengo ya uhakika kwa ajili ya taasisi yake, hivyo kulazimika kupanga katika majengo ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ambako baada ya kudaiwa kushindwa kulipa kodi, mali zake ikiwa ni pamoja na vifaa na samani zote zilizokuwa katika taasisi hiyo zilipigwa mnada. Baadaye aliripotiwa kuibuka upya na kuanza kuwekeza taasisi nyingine ya magonjwa hayo eneo la Mbweni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 18, 2013

    RIP fellow Dr, you can be proud that at least you tried to make a change in very difficult circumstances.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 18, 2013

    Poleni sana familia ya marehemu. Utakumbukwa kwa kazi kubwa sana uliyoifanya wakati wa uhai wako.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 18, 2013

    Pamoja na vikwazo vyote alivyowekea na baadhi ya viongozi serikalini lakini subirini muone salamu za kinafiki zitakavyomiminika kwa kumpamba kwa sifa mbalimbali ilhali wakati wa enzi za uhai wake hawakumpa msaada wowote na wao ndio walikuwa mstari wa mbele kumkwamisha asitimize malengo yake ya kuwasaidia wanyonge wasiokuwa na uwezo wa kwenda India kutibiwa.Shame on them

    ReplyDelete
  4. Poleni sana wanafamilia wa mpendwa wetu.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 18, 2013

    Alifanya alichoweza kuokoa maisha ya watanzania wasio na uwezo.mtu km huyu ndo anatakiwa kukumbukwa na tanzania I hope watatambua mchango wake ht baada ya kuondoka.rip unsang hero!

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 18, 2013

    sasa mtu mwema na mwenye malengo kama huyu anaondoka kabla ya kufikia malengo yake ya maana ktk jamii...mijitu ambayo haina mbele wala nyuma inaishi hadi miaka 100! watanzania kama tumelaaniwa hivi??

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 18, 2013

    R.I.P Dr.
    Ulijitahidi kuonyesha kwamba hata bongo inawezekana tukatibu magonjwa yetu sisi wenyewe lakini ulikwamishwa na wachache wenye uchu wa pesa hata kama itagharimu uhai wa mtu!

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 19, 2013

    shujaa halisi wa taifa...RIP

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 20, 2013

    POLENI BANA BASU, MRUTUNGURU NA UK YOTE. KUMBE WATU WA KULETA MAENDELEO KISIWANI WAPO HAWASIKIKI TU.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 20, 2013

    Salute comrade! You fought the good fight of FAITH! May the Almighty God prepare happy dwellings for you in Heaven of Heavens! & May your name Dr Masau remind us of HOPE forever. Long live LOVE! Long live TIH! True work stands the test of time. Watanzania wenzangu, tumefiwa jamani, poleni.

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 21, 2013

    Mungu amrehemu Dr Masau.alikuwa mtu ambaye amejitolea kuisaidia jamii yetu.Nakumbuka jinsi alivyokuwa anasema hapati kuungwa mkono vya kutosha na serikali katika kuiendesha hospitali.Najua wanafiki (SERIKALI) watasema tumepoteza lulu.Lakini cha kujiuliza ,ni kwanini mtu kama huyu mwenye msaada mkubwa kama huu,alikuwa hapati kuungwa mkono vya kutosha na serikali??
    Nakumbuka katika moja ya mahojiano yake,Hayati Dr Masau,aliwahi kusema kwamba kuna magonjwa mengi ya moyo ambayo yalikuwa yanatibiwa na hospitali yake na kilikuwa hakuna ulazima wa serikali kutumia mamilioni kupeleka watu India.
    Je lakini nani anajali???
    Inahuzunisha sana jamani!!!!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...